Magazine Sauti ya pwani 246 Final

Transcrição

Magazine Sauti ya pwani 246 Final
Vijana
wajitokeza
kujiunga na
huduma za
vijana picha
zaidi
uk. Wa 11
MASHAMBULIZI
Vurumai za Tana
Delta soma uk.
Wa 4
auti
ya
S
Pwani
Kichocheo Kwa Turathi Za Pwani
SAUTI YA PWANI Novemba 2012
Kandanda ya viziwi
yazindua
msisimko mpya
Na Paul Olale- Kaunti ya Kilifi
imu ya soka ya viziwi ya Malindi iliichabanga
timu ya viziwi ya Makupa PCEA, Mombasa, 3-0,
katika mchuano wa kirafiki katika uga wa
kijamii, mjini Mombasa.
Nyota ya mechi, Antony Kadenge, ndiye aliyejaza
wavuni mabao hayo yote matatu,
Katika kipindi cha pili Kadenge alilifunga bao la pili dakika
ya 47, na la tatu dakika ya 64.
Mechi hiyo iliwavutia mashabiki wengi mno, waliokuja tu
kuthibitisha kama kweli viziwi wengeweza kusakata soka
barabara.
Mechi hiyo ilikuwa mojawapo ya misururu ya michezo
ya viziwi yanayoendelea eneo la pwani , na
yaliyotayarishwa na ushirika wa viziwi nchini, tawi la
Malindi.
Mtayarishi wa michezo hizo tawi la Malindi, Bi Priscilla
Kibicho, alisema madhumuni yake ni kuihamasisha
umma kutambua uwezo na haki ya wale wenye ulemavu
mbalimbali,ili kwamba kusaidia kuondoa ubaguzi na
unyanyapaa.
Bi. Kibicho ana ulemavu wa kusikia, na ni mwalimu
walugha ya ishara ya viziwi, mjini Malindi.
KALOLENI WEMA BUTCHERY
Dondokwa na mate!!!
Nyama Bora
Iwe ni ya choma, chemsha au karanga
auti
ya
S
UTAIPENDA
Nambari zetu za simu
0728786868 0739820182
Pwani
Kichocheo Kwa Turathi Za Pwani
TOLEO NAMBARI 246
NOVEMBA 2012
BEI 30.00
YALIYOMO
?
Viongozi wataka amani
k. 10
?
Athari za ukame zazua maafak. 4
?
Kondoo mweusi atimuliwa kanisani uk. 12
T
Ahitaji msaada kugharamia uuguzi
Si vita… la hasha! Mchezo wa karate umenoga
katika Kaunti ya Kilifi, wakubwa kwa wadogo
Mashtuko baada ya mashambulizi ya Tana Delta
Ahitaji msaada
Vijana wakipokea tuzo na shani baada ya kushiriki kwenye
mchezo wa karate uliofanyika huko Kilifi hivi majuzi
Kutoka uk. Wa 8
na uharibifu wa viungo kuonekana hivyo basi
kuzusha kero baina ya jamii na ukosefu wa
fedha wakati wa kutaka matibabu.
Shirika la WHO linapendekeza kuwa
maeneo yote yaliyoathiriwa yatambuliwe ili
miradi ya matibabu ianzishwe na kutibu watu
wote wanaotishiwa na kuambukizwa kwa
matende kwa muda usiopungua miaka
mitano.
Njia nyingine ni kuwawinda na kuwazuia
mbu kusambaza viini kwa kutumia neti
zilizotibiwa.
Ingawa Abdalla hana ufahamu kuhusu
miradi ya serikali kuhusu tiba za matende,
ana matumaini kuwa siku moja atapata
wafadhili ili naye aweze kuishi maisha ya
kawaida tena.
Iwapo umeguswa na hali hii ya Abdalla na
ungependa kutoa msaada wa hali na mali
unaweza kuwasiliana naye kwa rununu
0724257376 au 07752551906 ama
uwasiliane na Abdalla Mwangade, Post
Bank-Ukunda Branch A/c 0428010090974.
Gazeti Hili Huchapishwa na Wizara ya Habari na Mawasiliano S.L.P. 421-Mariakani e-mail: [email protected]
Na Nyambura Ngugi na Abdullahi Hussein, Kaunti ya
Mombasa
Yusuf Abdalla ni mzaliwa na mwenyeji wa Pwani ambaye
amekuwa akiugua ugonjwa wa matende kwa zaidi ya miaka
13 sasa. Madaktari wamemtangazia kuwa mguu wake wa
kushoto hauna manufaa kwake tena kutokana na athari za
ugonjwa huo na njia iliyobakia ni kuukata.
Haya ndiyo masaibu yanayomkumba na anahitaji kwa
dharura msaada wa kimatibabu na fedha ili atimiziwe
matibabu ya kukatwa mguu.
Kulingana na wauguzi matende husababishwa na aina ya
minyoo ambayo hufurisha miguu na mikono na hata sehemu
nyeti za wanaume.
Inaendelea uk. Wa 8
Wafanya Ngono Hadharani
Taarifa ya Rajab Ramson Mzee
na kuandikwa na Paul Olale
Kaunti ya Kilifi
W
anaume wawili waimbaji
nyimbo za kitamaduni ya
Kigiriama (msego),
waliafikiana kwamba iwapo mmoja wao
atakufa basi atakaye bakia afanye
mapenzi na mke wa mweziwe juu ya
kaburi baada ya mazishi, la sivyo
atakayekaidi afe pia.
Kwa hivyo hivi majuzi siku hiyo ilitimia
baada ya mwimbaji aliyetoa wazo hilo
kuaga dunia akiwa na umri wa miaka
48,kijiji cha Mpirani, kata ya Gongoni,
wilaya ya Magarini.Kakaze marehemu
walisisitiza ahadi hiyo lazima itimizwe.
Kwa hivyo ilivyo kawaida ya matanga
katika maeneo haya, pombe ya mnazi
uliletwa, na watu kubugia kwa fujo.
Marehemu alizikwa saa nane mchana,
nakuwekwa kando kando ya
kaburi.Mzee mmoja kisha aliwaamuru
wanawake kuchangia leso zao, ambazo
zilitundikwa kwa vijiti vile na kuuzingira
kaburi.
Basi mjane wa marehemu, miaka 36,
na yule mwimbaji walisukumwa ndani ya
pazia zile, na kuagizwa kufanya mambo.
Baada ya dakika kumi vishindo za
mateke kwenye zile leso ziliashiria
kwamba kazi ilikuwa ikiendelea, na watu
wakaanza kupiga makofi na
kuwamiminia sifa wawili hao, kwa
majina ya matani.
Dakika kumi zaidi, kwa sababu
walikuwa juu ya mchanga wa kaburi usio
thabiti, waliteremka hadi ukingo wa
pazia, na miguu yao yakaanza
kujipenyeza katika mianya ya leso.
Baadhi ya wazee walihofia kuanguka
kwa ua wa leso na kuwaacha uchi, na
wakamfokea jamaa yule kutozidisha
mpira, kwani uwanja ulikuwa mdogo.
Mechi hiyo ya ajabu ilichukua nusu saa,
na kisha mume alijitokeza kwenye
uwanja wa kaburi amelowa jasho kama
aliyeoga, huku akichechemaa kwa
uchovu.
Mke naye alibakia kule ndani, hadi
wanawake watatu wakongwe
walipongia pale na kumnyanyua na
kumpeleka kumlaza chumbani.
BUTWAA NA AIBU
Haikujulikana mara moja
kilichomtendekea; pengine uchovu,
kupigwa na butwaa, aibu, ulevi au
mchanganyiko wa vyote.
Baada ya hapo shughuli ya matanga
ziliendelea kwa siku tatu, na
waliosisimuliwa na tukio hilo
wakachangia’ombe watatu na mbuzi
waanne wakachinjwa, na mitungi 20 ya
mnazi kumiminwa. Kisa hicho kimebakia
kama ngano katika ndimi za watu wa
sehemu hiyo, kwani ni cha kwanza
kutendeka.
Gazeti hili hufikia kaunti za: Mombasa, Kwale, Kilifi, Lamu, Tana River na Taita Taveta
TAITA FEEDS
MANUFACTURES OF:
MINISTRY OF INFORMATION AND
COMMUNICATIONS
GROWERS, LAYERS, CHICK AND BROILER MASH
& SUPER DAIRY MEAL
LOCATED AT MCHARO’S BULIDING,
SHIGHARO ROAD.
DEPARTMENT OF FILM SERVICES
OFF WUNDANYI BUS TERMINUS
ADVERTISEMENT
P.O. BOX 1128 WUNDANYI
CELL: 0722 796 783/0738 402 231/0722 971 622
Email: [email protected]
For affordable prices and
door step delivery of all livestock feeds.
Targeted people include, Commercial
Photographers, Video/Studio operators/ Film
Makers both local and
International.
Please note that it is now mandatory under cap 222
of Film and stage plays act to first obtain a film
license before
engaging in any film production or practice.
Please visit the department of film services offices
located at SAUTI House, First floor, Mombasa City
or any Information office near your area for more
information.
You can be licensed as an Individual or as a Group
14
Sauti Ya Pwani
3
Sauti Ya Pwani
KAUNTI YA KILIFI
KAUNTI YA KILIFI
Bustani ya mimea asilia yaanzishwa Pwani
Na Irene Agum, Kaunti ya Kilifi
ustani kubwa inayojumuisha
aina zaidi ya 10,000 ya mimea
asili ambayo ilianzishwa
hapa Pwani kwa takriban shilingi
milioni tano sasa imefunguliwa
rasmi katika chuo kikuu cha Pwani
kilichoko mjini Kilifi na kutoa
changamoto wa mwanzo wa
ubunishaji wa mazingira bora hapa
Pwani.
Bustani hii iliyobuniwa kwa ushirika
wa Chuo cha Pwani, shirika la kitaifa la
mazingira, NEEMA na Shirika la
kimataifa la DANIDA litatumiwa kama
ghala la kuhifadhia aina mbali mbali ya
mimea kote duniani ikiwa ni pamoja na
ile mimea inayotishiwa kuangamizwa.
Bustani hii inatarajiwa kuwanufaisha
wanasayansi na wachunguzi wa
mimea na hali kadhalika kuwa kivutio
cha watalii hasa ikiangaziwa
mwelekeo wa kupandwa katika
sehemu mbali mbali ikihusisha mimea
inayofikiriwa kuwa na uwezekano wa
kutibu magonjwa, kuwa na mbao bora,
B
aina ya mimea isiyokuwa ya kawaida,
ile iliyo na manukato, vyakula na vile
vile ile inayotumiwa kama vivutia
macho.
Kwa sasa mmea kama vile ‘vilua’
ambao unakuzwa kwa wingi hapa
Pwani, unafanyiwa majaribio ili
uhusishwe kwenye viwanda vya
virembesho kutokana na ubora wa
manukato yake. Bustani hii inatarajiwa
kuwa na mimea aina nyingi zaidi hapa
afrika.
Nchi ya Kenya inakisiwa kuwa na aina
zaidi ya 100 zinazoorodheshwa kama
aina ya ‘aloe vera’ na ambazo
zinavunwa kwa kasi kiasi cha kutishia
kuangamizwa, kulingana na Dkt.
Mohamed Pakiya ambaye ni mtaalam
mkuu wa bustani katika Chuo kikuu cha
Kilifi.
Bustani hii pia inatarajiwa kubadilisha
hali ya maandhari ya Kilifi kutokana
kuletwa kwa aina ngeni za mimea
kutoka sehemu nyingine za dunia.
Uzinduzi wa bustani hii hapa Pwani
ulioongozwa na kaimu mwenyekiti wa
NEEMA, Bi. Kulamo Bullo ulikuwa
chanzo cha kubuni mwongozo mahsusi
wa maendeleo hapa Pwani. Mwongozo
huu utawezesha ukufunzi wa mawazo
na uchunguzi kunufaisha jamii moja
kwa moja baada ya kuwajumuisha.
Kulingana na msimamizi wa Chuo
hicho, Profesa Mohamed Rajab,
mwongozo huo unatoa mikakati ya
utekelezaji ikiwa ni pamoja na mbinu za
kuendeleza miradi na mipangilio katika
chuo. Haya yanatarajiwa kuwa
sambamba na mipangilio ya Chuo
kama michango ya kuendeleza elimu
kwa maendeleo ya kitaifa.
Elimu kwa maendeleo ya kitaifa (ESD)
ni mbinu zinazotumika kufundisha na
kusoma zinazoegemea kujitegemea;
jamii zinatarajiwa kubuni ari ya
masomo, ujuzi na elimu ya kuendeleza
bila kuvuruga vizazi vijavyo
kujiendeleza..
HALISI COMMUNICATIONS
Your professional Consultants in Printings, Video & Photo productions, Media, IT and Capacity Building.
GOODS/SERVICES
1. DESIGN, TYPESETTING &PRINTINGS: T-shirts, Magazines, Newsletters, logos, posters,
signboards, cards, receipts etc.
2. PRODUCTION: Video shooting & Editing for news, corporate affairs, weddings, ceremonies,
documentaries etc. Photography & Digital Imaging; for all types of occasions and purposes.
3. EVENTS MANAGEMENT: Tents, chairs, sound systems, lighting, catering for HIRE.
4. SUPPLIES: Stationery, toners, cartridges, computers, laptops and accessories, tree seedlings and flowers,
printed exams for primary & secondary schools.
5. TECHNICAL & MEDIA: IT solutions, computer repairs and maintenance, web designs and
programming, news and features services for radio, TV, print and online publications and social media.
6. TOURISM: In partnership with Mlilo Community Tours& Safaris. Bookings, tour guiding, provision of
camping sites home stays for ecotourism within rural communities. Video productions and photography for
tourism experiences and promotions.
7. CAPACITY BUILDING: On-job, on-site and in-house trainings in community development issues,
proposal writing, community tourism enterprises, internship for tourism and media students, project
management, mentoring and motivational speaking.
Network across East Africa- Kampala, Busia (U&K), Malaba, Kakamega, Mumias, Kisumu, Mwanza
(Tz), Nairobi
Malindi branch- Malindi-Lamu Rd.
Contacts – Latifah Abdallah (Nidhamia Hall) -0707-956592
Musyoka A - 0710-335833
Bernard - 0710-996042
Livingstone - 0712-340875
Albert - 0724-539302
Kustawisha
Uvuvi
kazkazini
mwa Pwani
Na Irene Agum, Kaunti ya Kilifi
h a b a w a s a m a k i
unaosababishwa na vifaa vya
uvuvi duni unadaiwa
kusambaratisha juhudi za kuanzisha
mitambo ya biashara ya samaki wa
mikebe huko kazkazini mwa Pwani.
Mitambo miwili iliyoko sehemu hiyo
imekuwa ikifanyiwa kazi ndogo ndogo
kwa vile wavuvi katika sehemu hiyo
wameshindwa kuvua samaki
wakutosha.
Mitambo hiyo ikiwa na uwezo wa
kusaga na kuhifadhi samaki tani 12,000
kwa siku katika kampuni ya Diamond
Sea Food Limited inalazimika kufanya
kazi kati ya mwezi wa Oktoba na Machi,
ikisaga na kuhifadhi tani tano pekee
ambayo haifikii hata nusu ya uwezo wa
mitambo yake.
Hii inatendeka katika sehemu iliyo na
maeneo makubwa ya samaki ambayo
yana uwezo wa kuipatia nchi hii zaidi ya
shilingi milioni 75 kila mwaka.
Wavuvi hata hivyo wameiomba serikali
iwasaidie kuongeza viwango vyao vya
kuvua samaki kwa kuwapatia meli
kubwa zitakazowawezesha kuvua
samaki kwenye maji marefu badala ya
kutegemea kujenga mabohari.
Wavuvi hawa wanasema kuwa mahitaji
ya samaki yamekua kwa kiwango
kikubwa hata baada ya kubuniwa kwa
kilimo cha kufuga samaki na kuwa
sehemu nyingi za uvuvi bado hazivuliwi.
Akizungumza na vyombo vya habari
huko Mtwapa, mkurugenzi mkuu wa
Diamond Sea Foods Limited, Bw.
Mohamed Khizer alisema wingi wa
samaki katika maeneo yaliyopakana na
Somalia kama vile Lamu, Malindi,
Watamu na Kilifi imedhihirika lakini
ukosefu wa meli za kuvulia umewafanya
wavuvi kusalii amri na kushindwa
kuendeleza uvuvi.
Kwa sasa kuna meli moja tu yenye
uwezo wa kuvua maji marefu.
U
Daktari wa macho akishughulikia moja ya wateja wake
Afya ya jamii yakumbwa na
matatizo ya usafiri
Na Irene Agum, Kaunti ya Kilifi
atizo la usafiri linaendelea kuwa
k i k w a z o k i k u b w a
kinachochangia kuzorota kwa
afya ya jamii katika kaunti ya Kilifi.
Barabara duni na vituo vya afya
vilivyojengwa mbali vimesababisha
wanawake wengi kuzalia majumbani
mwao ilhali wengine wao hujitosa kwa
waganga wa kienyeji ingawa wizara ya
afya inafanya kila jitihada kuboresha
huduma za matibabu kote nchini.
Watu wengi wanaozuru zahanati kwa
matibabu wana dhana kuwa wauguzi ni
wale ambao bado wako mafunzoni na
wanaaihimiza serikali kuwatuma
wauguzi waliohitimu katika zahanati
hizi za Kaunti ya Kilifi.
Wanawake wanaonekana kuwa na
wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa
muda wa ‘uchungu’ wakati wa kuzaa
ilhali wengine huwa wanapatwa na
matatizo ya kubaki na ‘mji’ au nyumba
ya mtoto jambo ambalo linachukuliwa
kama mkosi baina ya wanawake
waoga katika kaunti hii.
Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni
umeonyesha kuwa itikadi na mila katika
sehemu nyingi za kaunti ya Kilifi
zimewafanya wanawake wengi
kususia kupimwa kabla na baada ya
kuzaa na badala yake kutegemea
huduma za wakunga wa kienyeji.
T
Uchunguzi huu umependekeza
kuwa wakunga wa kienyeji na wale
wazazlishaji waliostaafu waruhusiwe
kuendeleza huduma zao kwa vile
wamekuwa wakitegemewa pakubwa
kutokana na itikadi na mila zilizokithiri
miongoni mwa wakaazi wa kaunti ya
Kilifi.
Uchunguzi huo uliofanywa na
shirikia lisilokuwa la serikali, Kwetu,
lilichukua muda wa miezi sita na
limegundua kuwa gharama kubwa ya
usafiri na umbali wa zahanati
unawanyima fursa ya kupata huduma
za matibabu.
Uchunguzi huo ulidhamiriwa
kutafuta chanzo cha kuzorota kwa
idadi ya watu wanaopokea huduma
za matibabu.
Akipokea ripoti hiyo ya uchunguzi
kutoka kwa afisa wa haki za
binadamu, Bi. Joria Suud, mkuu wa
matibabu wa Kilifi Dkt. David Mulewa
alidokeza kuwa ingawa kuna
changamoto nyingi kutokana na
upungufu wa wauguzi amekuwa
akiwahimiza vijana wengi walio na
kisomo kujiunga na Taasisi ya
matibabu (KMTC) ama Chuo kikuu
cha pwani ambavyo vinatoa shahada
za uuguzi hapo Kilifi.
4
Sauti Ya Pwani
Tahariri
KAUNTI YA LAMU
UPOFU
Huku ulimwengu mzima ukiadhimisha
siku maalum iliyotengwa kuangazia
kutunza macho, wenyeji wa kaunti ya
Kilifi na vitongoji vyake hawana lolote
lile la kufufahia kwa vile wanaendelea
kukumbwa na matatizo ya macho.
Kwa wale wachache ambao hujitahidi
kusafiri mwendo mrefu ili wapate
matibabu ya macho Katika hospitali
kuu ya Kilifi ni kero kwani kuna daktari
mmoja tu ambaye hutibu watu siku
mbili tu kila wiki.
Ukifika kwenye zahanati
inayoshughulikia macho utakuta
milolongo mirefu ya wagonjwa wa
macho ambao wengi wao huambiwa
waende kwa matibabu Katika hospitali
kuu ya mkoa wa Pwani mjini Mombasa,
ilhali wengine wamejulikana kuwa
vipofu kwa ugonjwa ambao ungetibika
iwapo wangemuona daktari wa macho
kwa wakati ufaao.
Kulingana na Dkt. David Mulewa
ambaye ndiye mkuu wa matibabu
Katika hospitali kuu ya Kilifi, huduma ya
matibabu ya macho inakumbwa na
uhaba wa madaktari waliohitimu
taaluma ya macho na anawaomba
washirika na wadau kujitokeza
kuisaidia hospitali ya Kilifi kukabiliana
na tatizo hilo.
Kati ya maradhi yaliyopokewa Katika
hospitali hii ni pamoja na viini
vinavyosababisha upofu hasa Katika
watoto; inakisiwa kuwa zaidi ya watu
milioni 18 wamepofuka duniani ilhali
ugonjwa huu una tiba.
Inadaiwa kuwa watoto ndio walio
kwenye hatari ya kuambukizwa na
hivyo basi kuchangia kuendeleza
umaskini baina ya jamii.
Wakati wa kliniki ya bure iliyofanyika
Katika kanisa la Katoliki la Kilifi,
madaktari walionya kuhusu ugonjwa
wa kisukari kama moja ya sababu
zinazoleta upofu.
Daktari mmoja wa macho kutoka
Mombasa, Dorcas Njuguna anasema
kuwa kisukari huambukiza mishipa ya
macho na kumfanya mtu kuona vugu
vugu na kuwa kipofu bila kutambua
kwa vile haina maumivu.
Ni dhahiri kuwa ugonjwa huu una
madhara na wito wetu ni kuwahimiza
wananchi kuhudhuria kliniki mara kwa
mara ili wajijue hali zao za kisukari na
macho ili janga hili liweze
kuangamizwa.
Athari za ukame zazua maafa
Na David Mutwiri
na Jackline Wambui,
Kaunti ya Lamu
aunti ya Lamu, kwa muda
mrefu sasa, imekuwa kimbilio
na mokozi wa jamii za wafugaji
kutoka maeneo ya kazkazini mwa
Kenya wakati wa kiangaza lakini
maendeleo ambayo yanajiri kutokana
na kuanzishwa bandari mpya
yaonekana kukatiza maeneo ya
malisho na hivyo basi kuzusha
taharuki kati ya binadamu na
wanyama, jambo ambalo
limeshuhudia vifo vya watu wengi
huku wengine wengi wakijeruhiwa.
Taharuki ya binadamu na wanyama
ilizidi na kufikia viwango vya kutisha
baada ya vurumai za Tana Delta
ambazo zilisababisha jamii kutorokea
usalama wakiambatana na makundi
makubwa ya mifugo na hivyo basi
kuongezea uhasama ambao ulikuwa
unasababishwa na jamii za
kuhamahama kutoka wilaya jirani za
Ijara.
Hali hii inazidi kuwa mbaya kutokana
na kubuniwa kwa maeneo ya ufugaji
ambayo yamewawekea vikwazo na
ku z i b a n j i a a s i l i a wa l i zo ku wa
wakizitumia wafugaji wa
kuhamahama.
Baadhi ya maeneo haya ya ufugaji
hayaeleweki, wala mipaka yake
haijulikani na yanadaiwa kumilkiwa na
mabwenyenye waliolenga upanuzu na
maendeleo yaliyoletwa na ujenzi wa
bandari ya Lamu.
Maeneo ya kazkazini mwa Kenya
yanajulikana kwa kukumbwa na janga
ukame lakini shida ni kuwa bado
hakujapatikana suluhu bayana kwa
tatizo hili sugu.
Eneo hili kame linalopakana na nchi
jirani inayokumbwa na vita vya mara
kwa mara ni makaazi ya jamii ya
wafugaji wa kuhamahama ambao
wana sifa za kufuga wanyama wengi
ambao huwalazimu kuhama kutoka
eneo moja hadi lengine wakitafuta
K
Uhamaji wa mara kwa mara wa
wafugaji hawa umekuwa ukiendelea
kutoka miaka ya sabini huku mifugo
ikiingia Lamu kutoka maeneo jirani ya
Garissa, Tana Delta, Bura na hata Ijara.
Baadhi ya wafugaji hawa
walikumbana na ubatili wa maendeleo
mapya hivi majuzi wakati walipojaribu
kuingiza mifugo wao kutoka Ijara na
kukatazwa ikidaiwa kuwa maeneo hayo
yalikuwa ni mali ya mtu binafsi. Jambo
hili liliwafanya wafugaji hao kupoteza
zaidi ya ng’ombe 40 baada ya kukosa
malisho na maji kwa zaidi ya siku
kadhaa.
Huku suluhu kwa matatizo haya
yakiwa kitendawili, wafugaji hawa
wamejikuta kwenye njia panda na
kukorofishana na wakulima ambao
wanadai mifugo inawaharibia mimea
yao.
Wakati wa uhamisho, makundi
makubwa ya ng’ombe hujaribu kunywa
maji kwenye visima vilivyo katikati ya
mashamba. Kwa makundi ni makubwa
na wachungaji ni wachache, ng’ombe
hugeukia mazao ya wenyewe na
kusababisha uharibifu na kuzua
farakano.
Ni kati ya hali hizi zisizofurahisha
kuendelea uk. Wa 5
13
Sauti Ya Pwani
Mazuia maji yajengwa Pate
na Ndau
Na David Mutwiri, Kaunti ya
Lamu
haribifu wa vifaa na bidhaa
unaosababishwa na
mawimbi mazito ya Bahari
katika maeneo kadha ya siwa la
Lamu yatazikwa kwenye kaburi la
sahau baada ya serikali kutumia
zaidi ya shilingi milioni 364
kujenga mazuia na kuta katika
visiwa vya Pate na Ndau.
Mradi huo ulihusisha ujenzi wa
ukuta wa mita 1400 kwenye kingo za
Bahari za Faza katika kisiwa cha
Pate na zuia la mita 420 katika kisiwa
kidogo cha Ndau mashariki mwa
kaunti ya Lamu.
Mheshimiwa Chris Obure, ambaye
ni waziri wa Ujenzi wa kitaifa
alidokeza kuwa ujenzi wa kuta la
Faza na lile zuia la Ndau ziko kwenye
vitengo vya maendeleo viitwavyo
“kazi nyingine za taifa”
vinavyoshuhulikia ujenzi na
ukarabati wa madaraja madogo, kuta
za Bahari, vituo vya kuegesha
madau na mazuia.
“Hapo awali maji ya Bahari yalikuwa
kero kwa vile wakati maji yanapojaa,
mawimbi mazito yalikuwa
yakisukumwa hadi ndani ya nyumba
na kuharibu mali na kuwa kero kwa
wenyeji wakati wanapotembea au
kufanya kazi kwenye ufuo wa Bahari
U
wa Faza,” akasema Obure.
Waziri huyu aliyasema hayo wakati
wa hafla ya kupokea mradi wa Faza
iliyofanywa hivi majuzi. Ujenzi wa
kuta la Faza na lile zuia la Ndau
zilianza kujengwa kuanzia mwezi wa
Oktoba 2007 na ulitarajiwa
kukamilika Agosti 2010.
Serikali pia imetenga shilingi milioni
42 zitakazogharamia ujenzi wa kuta
katika kijiji cha Kizingitini. Mradi huo
utakaojumuisha njia badala ukingoni
ya kilomita 1.35 sambamba na kikuta
cha Ndau inatarajiwa kukamilika
mwezi wa Julai 2013 kulingana na
mhandisi wa wizara ya ujenzi,
Mhandisi Benjamin Mwangi.
Takriban mita 5,000 za kuta katika
fuo za Bahari zimejengwa na
kukarabatiwa katika kaunti ya Lamu
toka mwaka wa 2003 ili kuchangia
maendeleo ya kiuchumi na hasa
mawasiliano ili kuwasaidia wenyeji
kutimiza malengo ya riwaza ya kitaifa
ya 2030.
Ujenzi wa kuta za baharini
unafaanywa na kampuni ya
Associated Construction Company
Limited ikisimamiwa na tume ya
usimamizi ya
wizara ya Ujenzi.
Wizara hiyo pia itatumia shilingi
bilioni 1.2 kukarabati kiegezo cha
SAUTI YA PWANI
EDITORIAL
Ag. Editor:
Hussein Abdullahi
FIELD EDITORS
Simon Guruba:
Daniel Mwangi:
Mercy Ndirangu:
Irene Agum:
Paul Olalo:
Emmanuel Masha:
Mutiso Mbithi:
Wundanyi
Voi
Kwale
Kilifi
Malindi
Hola
Lamu
PRODUCTION
Safari Baya:
Mariakani
ADVERTISING RATES
Full page
Half page
1/4 page
1,000.00
600.00
400.00
Kambi ya muda iliyobuniwa kufuatia uvamizi huko Tana Delta.
Jamii kadhaa zililazimika kukimbilia usalama baada ya
uvamizi uliosababisha maafa na majeruhi
KAUNTI YA LAMU
madau ili kuboresha biashara za utalii
katika sehemu hiyo.
Habari zaidi zasema kuwa Wizara
ya ujenzi inanuia kufanya michoro ya
kiuhandisi itakayokuwa na mitindo
sawa kwa mijengo yote ya makao
makuu ya kaunti kote nchini ili kuwe
na usawa katika ugavyi wa mamlaka
ya serikali.
Waziri Obure huku akitoa agizo kwa
mchoraji rahamani mkuu katika
wizara yake kuhusu mtindo wa
majengo yatakayoptumika kwa
wakuu wa kaunti, alisema kuwa
anafadhaishwa na jinsi wizara
nyingine zinavyojenga maofisi
kiholela bila kushauriana na wizara
yake.
Obure, ambaye alikuwa
amemtembeelea Mkuu wa Kaunti ya
Lamu, Stephen Ikua alisisitiza kuwa
wizara yake itahakikisha kuwa kuna
usawa wa mitindo ya majengo ya afisi
zote nchini na kuhakikisha kuwa
yamejengwa kwa viwango vya juu
vya kuridhisha ugatuzi.
“Nikiwa kwenye wizara iliyopewa
jukumu la upangaji, uchoraji, ujenzi
na hata kukarabati rasilimali za
serikali, nitajitahidi kuhakikisha kuwa
mahitaji ya miundo misingi ya ujenzi
katika kila kaunti inatimizwa ili kukuza
uchumi wa kitaifa,” akasema Mhe.
Obure.
Waziri huyo alidokeza kuwa wizara
yake imesimamia ujenzi wa zaidi ya
majengo 750 ya wizara mbali mbali
humu nchini na pia kukarabati miradi
zaidi ya 222 kupitia kwa kitengo cha
wizara yake kinachosimamia
uboreshaji na ukarabati wa majengo
ya serikali.
“Wizara yangu pia imesimamia
ujenzi unaohusisha sekta mbali mbali
kama vile mashule, hospitali, sekta
ya kilimo na kukamilisha majengo
210 kati ya 226 yaliyokuwa
yamekwama katika sehemu mbali
mbali humu nchini,” akaongeza Bw.
Waziri.
Alitangaza kuwa wizara yake
itatenga zaidi ya shilingi milioni 30
kugharamia ujenzi wa makao makuu
ya Faza katika kaunti ya Lamu.
12
Sauti Ya Pwani
5
Sauti Ya Pwani
KAUNTI YA TAITA-TAVETA
KAUNTI YA TAITA-TAVETA
Wafugaji watahadharishwa kujiandaa kwa ukame
Na Wagema Mwangi,
Kaunti ya Taita Taveta
dara ya Ufugaji wilayani
Mwatate katika Kaunti ya Taita
Taveta imetoa tahadhari
huenda kukawa na ukame wa
muda mrefu baada ya mabwawa
kukauka kufuatia kiangaza
kikali.
Maeneo mengi katika wilaya hii
inayojulikana kuwa eneo kame,
kwa muda wa miezi mitano iliyopita
imekumbwa na uhaba wa maji hali
ambayo imesababisha kumalizika
kabisa malisho katika eneo la
malisho.
Huku mifugo wadogowadogo
wakiendelea kustahamili, afya za
wale wakubwa kama vile ng’ombe
zinaendelea kuzorota na kutoa
tisho huenda wafugaji wakapata
hasara kubwa kutokana na maafa
ya mifugo wao.
Akizungumza na mwandishi wetu,
afisa mkuu wa mifugo wa wilaya ya
Mwatate, Bw. Martin Oyindo
alisema kuwa sehemu zilizoathirika
zaidi ni pamoja na Mwakitau,
sehemu za Mwatate na
Kamutonga.
Alisema kuwa mvua ambazo
zimekuwa haziaminiki toka mwezi
wan ne imesababisha nyasi
kukauka kwenye maeneo kadha ya
malisho na hivyo basi kuwafanya
wafugaji kuwa na fedheha kwa
mipangilio ya siku za usoni.
“Tuna wasi wasi mkubwa kuhusu
mifugo wetu kwa siku zijazo.
Mabwawa yote sasa yamekauka
ilhali mvua nazo bado hazijaanza
kunyesha kama tulivyotarajia,”
akasema Bw. Oyindo.
Afisa huyo aliwashauri wafugaji
walio na makundi makubwa ya
mifugo wachukue hatua za haraka
za kuwauza huku masoko yakiwa
na bei nzuri na akasisitiza kuwa ni
bora kuwa na mifugo wachache
ambao
watawashughulikia vyema wakati
I
huu wa kiangaza.
Alidokeza kuwa wafugaji
wamekuwa wakiwapoteza mifugo
wao wakati wa kiangaza na
akaonya kuwa hali hiyo itajiri iwapo
wakulima hawatachukua hatua za
haraka kuwapunguza mifugo wao.
“Ni lazima tuwauze mifugo wetu
wa ziada ili tuepuke kupata hasara.
Tutakuwa na fursa ya kununua
wengine wakati mvua inyeshapo,"
akasisitiza.
Hali hii ya upungufu wa mvua
inazidi
kuwa mbaya, kwa vile inawalazimu
wenyeji kufunga safari ndefu
wakitafuta maji kwa matumizi yao
na vile vile kwa mifugo wao na mara
nyingi kuuziwa kwa bei ghali mno.
Idara ya hali ya anga ilikuwa
imetoa tahadhari kuwa huenda
kukawa na mvua nyingi kuanzia
mwwezi wa Oktoba lakini hali hii
bado haijaonekana katika sehemu
kadha za nchi.
Fika Mnarani, Kilifi kwenye makavazi uone moja la pango la watumwa
Kondoo mweusi atimuliwa kanisani
Na Salome Mbeyu Tsuma- Kaloleni
K
ijana mmoja ametimuliwa na
mchungaji kanisani, kwa
kukosa kujirekebisha kutokana
na ‘mrundiko wa dhambi’.
Mchungaji George Tsuma, wa kanisa
la Rehoboth Fellowship katika kijiji cha
Chandoni wilayani Kaloleni, alimtimua
Collins Lisambu, mwenye umri wa
miaka 19, kwa madai ya wizi na ulevi,
miongoni mwa mengine.
Katika tukio la hivi karibuni, Lisambu
anasemekana, aliiuza
pikipiki ya muumini mmoja wa kanisa
hilo, baada ya kumwomba kutumia.
Mchungaji huyo alisema kadhalika
waumini walichoshwa na tabia yake ya
kuja kanisani akiwa mlevi,
kuwatongoza wasichana pale, na
kuhusishwa na visa kadhaa vya wizi.
‘Alikuwa fedheha kubwa kwa kanisa
kwa sababu kila mara anaposhikwa na
polisi kuhusiana na uhalifu, sisi ndiyo
tunaotoa faini kumaliza mambo hayo.
Sasa akishikwa kanisa halitahusika’,
alisema Tsuma.
Shirika la Huduma za Wanyama Pori kuimarisha elimu Taita
Na Simon Guruba, Kaunti ya Taita
Taveta
hirika la huduma za wanyama
wa pori (Kenya Wildlife
Service) limetumia takribani
shilingi milioni thamanini
(sh80million) kufadhili miradi ya
elimu tafauti tafauti katika Kaunti ya
Taita Taveta ili kuinua viwango vya
elimu katika eneo hili.
Miradi hii ni kama Mwaktau youth
polytechnic, Kiangachini nursery
school, Manyani, Mwamunga, Mulilo
primary schools na madawati kwa shule
ya msingi ya Kishushe.
Pia mwaka wa 2004 shirika la KWS
lilifadhili ujenzi wa madarasa mane, afisi
ya mwalimu mkuu na chumba cha
walimu (staffroom) katika shule ya upili
ya Mwaktau.
Akianzisha rasini ujenzi wa bweni la
wasichana katika shule ya Mwakitau
ambalo ligarimu shilingi milioni mbili
nukta inne (sh2.4m) na kufadhiliwa na
shirika la huduma za wanyama wa pori,
naibu wa mwenyekiti wa bodi la huduma
la udhamini la wanyama wa pori (KWS
Board of Trustee) ambaye pia ni
mkurugenzi katika bodi hiyo Bi.
Margaret Mwakima alisema shirika la
KWS limejitolea kuinua kiwango cha
elimu na maisha ya jamii za Taita Taveta
Kauti.
Akiongea hapo shuleni hivi majuzi Bi.
Mwakima alisema shirika la KWS
linafahamu kwamba masomo katika
kata za Mwaktau na Mwachabo
hutatizwa sana na ndovu wakati
wanapo vamia sehemu hizo.
Akihutubia wazazi na wanafunzi wa
shule hiyo Bi. Mwakima alisema ili
kuhakikisha kwamba Kaunti ya Taita
Taveta inashindana vyema kielimu na
maeneo mengine nchini, shirika la KWS
litahakikisha kwamba visa vya uvamizi
ambavyo vinatekelezwa na ndovu ama
wanyama wote wa porini vinamalizwa.
Hali hii itaweza kuinua kiwango cha
elimu na kuhakikisha wanafunzi
wanaendelea na masomo yao shuleni
bila kutatizwa na ndovu kwa kuwazuia
ndovu kuwavamia kupitia ujenzi wa uwa
S
wa umeme.
Bi. Mwakima anasema “shirika la
KWS linasikitika sana kuona baadhi ya
shule hupunguza masaa ya masomo
wakati wanafunzi hu
lazimika kufika shule kuchelewa ama
kurudi nyumbani mapema kuhofia
uvamizi ama kushambuliwa na ndovu”.
Pia Bi. Mwakima alisema lengo la
shirika la KWS kujenga bweni katika
shule ya Mwaktau kutapunguza visa
vya wanafunzi kushambuliwa na
ndovu wakati wakitoka nyumbani
kwenda shule kwani watakuwa
wanabaki shuleni.
Anasema visa nya “watoto wa shule
kukosa kuendelea na masomo ya
shule za upili kwa sababu shule hizo
ziko mbali na upungufu wa wazazi ama
kushidwa kwao kuwapeleka watoto
shule vitapungua kwani shule ya bweni
iko karibu”.
Kwa wanafunzi, Bi. Mwakima alisema
ufanisi kwa masomo hayatokani tu
kupitia kwa majengo mazuri, walimu
wakutosha na vitabu bali pia
kunatokana na kiwango cha umasikini
katika jamii, afya ya wanafunzi,
mchango wa wazazi kwa elimu ya
watoto wao na pia uhusiano wa
wanafunzi kwa wanafunzi shuleni.
Alisema tabia kama uhusiano wa
kimapenzi kati ya wanafunzi
wasichana, ndoa
na mimba za
mapema na unywaji wa pombe kwa
baadhi ya wanafunzi vimechangia kud-
horora kwa kiwango cha elimu
katika Kaunti ya Taita Taveta.
Pia aliwahimiza wazazi
wajihusishe na masomo ya watoto
wao, waunge mkono miradi ya
elimu na kupitia kwa juhudi hizo
visa vya watoto kuacha shule
vitapungua na kuinua kiwango cha
elimu katika Kaunti hii.
Athari za ukame
Kutoka uk. Wa 4
ambapo wafugaji wa jamii za kisomali na
wakulima wa kaunti ya Lamu
walikutanishwa kwenye mkutano wa amani
hivi majuzi.
Hapo, Mkuu wa kaunti hii, Stephen Ikua
alikiri kuwa nyakati zimebadilika na hali ya
maisha pia zimebadilika.
“Maeneo makubwa ya malisho sasa
hayako tena kutokana na ongezeko la watu
jambo ambalo limezua vizazi vipya na
ongezeko la mifugo,” anasema Bw. Ikua.
Upungufu wa maeneo ya malisho,
anaongeza Bw. Ikua, yataendelea kupungua
zaidi hasa kutokana na ujenzi wa bandari na
kubuniwa kwa mji mpya wa kisasa.
Dalili za kupanuka kwa mji wa Lamu,
umewavutia wawekezaji wengi ambao
wanajaribu kukita mizizi ya biashara zao
wakijiandaa na yajayo ili wapate faida.
Wanafunzi wakiandaliwa kwa zoezi la kilimo bora
6
Sauti Ya Pwani
11
Sauti Ya Pwani
KAUNTI YA MOMBASA
KAUNTI YA MOMBASA
Lamu na utamaduni wake
Lamu: Mji ulojawa na utajiri wa utamaduni,
historia na mila
Na Nyambura Ngugi,
Kaunti ya Mombasa
wa muda mrefu, mji wa
L a m u
a m b a o
umeorodheshwa na shirika
la kimataifa la UNESCO kama
kitovu cha utajiri wa utamaduni,
historia na mila za jadi,
umeendelea kuwa kivutio kikuu
kwa wageni kutoka sehemu mbali
mbali humu nchini, hali kadhalika
wale wa kimataifa huku kisiwa
hicho kikitoa maandhari ya
kufurahisha na kuburudisha
kimaisha.
Barabara nyembamba, vichochoro
na kingo za bahari zilizojaa watalii na
wenyeji waliovalia mavazi
yaliyoegemea tamaduni za kiislamu
limekuwa jambo la kawaida.
Hali hii ya utajiri wa mila na desturi,
historia na majengo ya jadi ya
Kiswahili inajiri mjini Lamu kutokana
na wageni walioitembelea katika
karne za 13 wakiwemo Wareno na
Warabu.
Hata hivyo, baadaye makundi
mengine yakitalii yalijitokeza na
kuhamia mjini humo na kuingiza
tumbo joto utajiri huo baada ya
kuingiza desturi mbovu kama vile
utumiaji mihadarati, ukahaba na hata
ushoga.
Ingawaje Lamu ni eneo linalomilkiwa
na waislamu ambamo desturi hizo
zinalaaniwa na makundi yote ya watu
wakiwemo wakristo, wenyeji na hata
wageni wanaoishi humo, desturi hizi
zimekuwa zikiendelezwa pasipo
kujali, kwani huendelezwa kisiri ili
watu wasijue.
Tukitaka kufichua jinamizi hili,
mwandishi huyu alisafiri hadi kisiwani
Lamu, akachunguza kwa kina na
marefu na kutuandalia taarifa hii
maalum kuhusu ushoga.
Kutana na Simon, silo jina lake, lakini
akiwa mfanyi kazi anayewaelimisha
mashoga na mabasha (watu
wanaofanya mapenzi na wenzao wa
jinsia moja-MSMs) katika zahanati ya
hospitali kuu wilayani humo,
amejitolea kwa hali na mali kufunza
njia salama zakutumika wakati
wakufanya ngono.
Hakudhania kuwa kazi hiyo inge
K
hatarisha maisha yake kwani miezi
michache iliyopita, kundi la
wanakereketo waliivamia hospitali ya
Lamu kwa kuandaa warsha iliyonuiwa
kuwalenga mashoga jambo ambalo
lilidaiwa kuwa kinyume na maadili ya
wenyeji wa Lamu na ambalo
lingeendeleza jinamizi la ukahaba na
ushoga.
Simon anasema kuwa ingawa jamii
kubwa ya wakazi wa Lamu ni
waislamu, ukweli ni kuwa
haijakubalika kuwa mashoga na
mabasha ni binadamu wanaoishi
miongoni mwetu na kama raia
wengine wana haki ya kikatiba kupata
mahitaji ya kimatibabu ya kimsingi.
Simon amekuwa akijihusisha zaidi
na kuzuia kusambaa kwa UKIMWI na
kuwatunza waadhiriwa katika kaunti
hii na katika muda wa miaka mitatu
sasa, amekuwa akiwahamasisha
wenyeji kuhusu kufanya mapenzi
wakitumia kinga na kupimwa mara
kwa mara ili wajue hali zao kiafya.
Kulingana na takwimu za hospitali
hiyo, asili mia nne za watu huathirika
lakini huwa inaongezeka au
kupungua kutegemea wingi wa
wageni wanaoingia na kutoka Lamu.
Mila na desturi zinazokashifu ushoga
zimekuwa changamoto hasa
ikizingatiwa utoaji huduma za
matibabu kwani mashoga ndio walio
na idadi kubwa ya waathiriwa wa
UKIMWI, Simon alimwambia
mwandishi huyu kwenye majadiliano
ya moja kwa moja.
Imemchukua Simon zaidi ya miaka
miwili kukubalika na kujumuika na
mashoga kama mwalimu kuhusu
kinga na ngono.
Afisa huyu anadai kuwa viongozi
katika eneo hili hawajihusishi
kikamilifu kuendeleza mbinu za
kuzuia kusambazwa kwa UKIMWI na
hali hii imeifanya kazi yake ya
mafunzo kwa wakaazi kuwa ngumu
zaidi.
Ongezeko la ngono baina ya watu
wa jinsia moja limeongeza viwango
vya kuvunjika ndoa na watu
wanapojiingiza kwa ndoa nyingine
huchangia pakubwa uenezaji wa
UKIMWI kisiwani Lamu, anasema
afisa huyo.
Kutokana na hali hii, viongozi wa
Inaendelea uk. Wa 11
Vijana wajitokeza kujiunga na shirika la huduma za vijana
Chapati yazusha
Kizaazaa
Na Paul Olale –Kilifi Kaunti
ulitokea kizaazaa wakati
jamaa mmoja aliibiwa
chapati Na mwenzake katika
kituo cha kuuza pombe ya mnazi,
mtaa Maweni Mjini Malindi.
Wakati(jina la utani) alipotaka
kuondoka karibu saa tatu usiku,
alipigwa na butwaa kugundua
kwamba chapati haikuwepo kando
yake kwenye kiti. Kisha alimwarifu
Rukia, mwenye kituo hicho cha
mnazi (mangwe), amsaidie
kuitafuta. Alisemaamemuomba
rafikiye amnunulie chapati hiyo, ili
ampelekee mtoto wake upande
mtaaKisumu Ndogo, kama chakula
chake cha usiku.
Lakini wateja walipoulizwa juu ya
jambo hilo, hakuna aliyetoa habari
yoyote. Basi Rukia aliufunga
mlango wa kibanda hicho, na
akawaagiza mababe wawili
wawapekuena wanawake walio
kuwa wakinywa pombe pale ndani.
K
Afisa wa Shirika la huduma kwa Vijana akikagua mmoja ya vijana waliojitokeza
Lakini upekuzi huo kwenye mifuko,
ndani ya nguo na chini ya viti,
haikufua dafu.
Kisha jamaa mmoja alitoa wazo
kwamba watu wote wasimamishwe
kutoka kwa viti vyaowote
waliposimamishwa, Looo! Chapati
uliofungwa kwa gazeti ulionekana
kitini, ambapo kulikuwa
kumekaliwa naFagia (jina la utani).
Fagia alizomewa vikali na wateja
kwa tukio hilo, lakini akadinda kuwa
hakuhusika na kupotea kwa
chapati hiyo. Lakini alipokuwa
akidinda, hakuwa na habari
kwamba kulikuwa na ushahidi zaidi
ya kumhusisha; jamaa mmoja
alimulika kwa tochi suruali yake, na
sehemu ya makalio kulikwa na
baka la mafuta!
Agwambo alipandwa na hamaki,
na akairaruararua ile chapati na
kisha kuikanyakanyaga
mavumbini, na akachomoka pale
na kutokomea gizani.
Kutoka uk. Wa 6
kidini wamehusishwa na wanapewa
mafunzo maalum katika hospitali kuu ili
wasambaze umuhimu wa kupimwa
kabla ndoa na elimu hii pia
inasambazwa kwa maharusi kupitia
kwa viongozi wa kidini kabla ndoa
kufungwa.
Kwa vile mashoga wengine ni watu
ambao wameoa na wana familia, afisa
huyu huwa anaandaa vikao vya siri
katika hospitali ili kuwapa mafunzo
kuhusu kufanya ngono wakitumia
kinga. Vikao kama hivi vinadaiwa
kuhudhuriwa na zaidi ya watu ishirini
ingawa kuna duku duku kuwa huenda
wengi wao wamejificha baina ya jamii
na hivyo basi kukosa huduma hii.
Mashoga, kulingana na afisa huyu,
wamepangwa kimakundi kwa minajili
ya kutekeleza majukumu kama vile
kugawanya mipira ya kinga wakati wa
ngono, kutangazia raia umuhimu wa
kupimwa UKIMWI na vile vile
kuonyesha jinsi mipira ya kike na ile ya
kiume inavyotumiwa.
Ili kuwakinga na kejeli kutoka kwa
wenyeji mashoga hawa wamefunzwa
kuulaani ushoga na kuficha matendo
yao halisi ili wawashawishi wenzao
kuwa kamwe hawashiriki kwenye
vitendo hivyo, Bw. Simon akamueleza
mwandishi huyu.
Hata hivyo, mbali na kukejeliwa,
changamoto inayowapata ni pamoja na
upungufu wa mafuta ya kulainisha,
ukosefu wa matibabu wakati
wanapoambukizwa hali kadhalika
ukosefu wa ajira kwa vile wengi wao
hawana kisomo wala vyanzo vya
kuwawezesha kuanzisha biashara.
Mmoja wa mashoga hawa aliyekiri
kushiriki biashara hiyo alisema kuwa
alijikuta kisiwani Lamu akiwa ametoka
kwao, Nairobi. Alijitambua kuwa na jinsi
za kishoga alipokuwa na miaka 12.
Anadokeza kuwa wateja wake mara
nyingi ni wageni na hata watalii ambao
hutembelea Lamu kutoka sehemu
mbali mbali. Wengine ni watu walio na
familia zao hapa hapa mjini Lamu.
“Niliweza kuwatambua wakati wa
uvamizi wa hivi majuzi,” akasema.
Yeye huwa anakumbwa na matatizo
ya kuambukizwa magonjwa ya zinaa,
na anapokumbana na mteja
anayetumia madawa ya kulevya, basi
huwa anapewa kichapo mara nyingine
bila malipo.
10
Sauti Ya Pwani
7
Sauti Ya Pwani
KAUNTI YA KWALE
KAUNTI YA KWALE
Viongozi wataka amani idumishwe Kwale
Wakulima wataka pembejeo zipelekwe karibu zaidi
Na Khamis Mohamed,
kaunti ya Kwale
iongozi wawaomba wananchi
wa tarafa ya Kubo katika kaunti
ya Kwale kudumisha amani
wakati wa kampeni na uchaguzi mkuu
unaotarajiwa kufanyika mwezi Machi
mwaka ujao.
Akizungumza katika baraza huko
Shimba Hills, kamishna wa kaunti ya
Kwale Bw. Evans Achoki aliwataka
wakaazi kudumisha amani katika
sehemu hiyo kabla ya uchaguzi na
hata baada ya matokeo ya uchaguzi
huo kutangazwa.
“Nawataka mudumishe amani katika
uchaguzi na hata baada ya uchaguzi
nigependa mudumishe amani.”
Alisisitiza Bw. Achoki.
“Na amani huanzia na mtu nyumbani
kwake. Kwa hiyo, ukishindwa
kudumisha amani katika nyumba
yako, huwezi kulalamika ukosefu wa
amani katika jamii.” Aliongezea.
Vile vile, Achoki aliwataka wananchi
kushirikiana na vyombo vya usalama
na kuripoti mtu yeyote yule
watakeyemshuku kuwa huenda
Na Khamis Mohamed, kaunti ya Kwale
akulima wa maeneo ya Shimba Hills waitaka
serikali kuwapelekea mbolea hadi mashinani
karibu na mkulima ili wapate afueni kutokana
na kulipa gharama za usafiri.
Akiongea katika baraza huko Shimba Hills, Eliakim Muoka,
mwenyekiti wa wakulima katika sehemu hiyo aliishukuru
serikali kwa juhudi zake za kuhakikisha kuwa wakulima wa
Shimba Hills pia wanapata pemebjeo.
Vile vile, Muoka aliiomba serikali kuhakikisha kuwa
pembejeo, haswa mbolea, inapatikana karibu na mkulima ili
kumuondelea mzigo wa gharama ya kuisafirisha mbolea
hiyo kutoka mji wa Kwale hadi Shimba Hills.
“Mbolea ni pembejeo muhimu kwa kila mkulima na
hatuwezi kuwa na usalama wa chakula bila ya kutumia
mbolea. Kwa hiyo tuna imani kuwa afisi yako itatusaidia kwa
hilo.” Muoka alimwambia kamishna wa kaunti ya Kwale,
Evans Achoki aliyekuwa mgeni katika baraza hiyo.
Katika wakati ambapo taifa la Kenya linajitayarisha katika
kuupokea utawala wa ugatuzi, Muoka alifichua kuwa
hatarajii kuwaona wakaazi wa wilaya ya Kwalewakipiga
foleni wakipokea chakula cha msaada wakati serikali hiyo
itakapochukua hatamu.
Vile vile, aliomba kuboreshwa kwa soko la Mvindeni
V
akawa ma mpango wa kuvuruga
amani ili hatua za kumdhibiti ziweze
kuchukuliwa katika wakati unaofaa.
Kamishna Achoki, alitambua elimu
kama nyenzo ya kuhakikisha kuwa
jamii inapata amani na hivyo basi,
aliwahimiza vijana kujiendeleza
kielimu hadi katika daraja ya chuo
kikuu.
Zaidi, aliwakanya na tabia ya kuacha
masomo katika darasa la nane huku
akizidi kuwahimiza pia kutafuta ajira ili
kujikimu kimaisha.
Afisaa huyo wa utawala aliwaomba
wazazi nao kuipatiliza amani
iliyopokuwapeleka watoto wao shule
ili waweze kuja kuwafaidi katika
maisha yao ya baadaye huku
akitambua kuwa bila amani watoto
hawawezi kuenda shule na kupata
elimu.
Kamishna huyo pia alifichua kuwa
tarafa ya Kubo imekaa kwa mda sasa
bila kuwepo na mkuu wa tarafa. Hata
hivyo, alizidi kufichua kuwa serikali ipo
mbioni katika kuajiri wakuu wapya wa
tarafa ili kujaza nafasi zilizo wazi
nchini.
Ziara ya kamishna wa kaunti katika
tarafa ya Kubo iliwasilisha bishara
njema kwa wakaazi kuwa watapata
mkuu mpya wa tarafa hivi karibuni.
Vile vile, mwenyekiti wa kamati ya
amani na maridhiano katikaya Kwale,
Bw. Jackson Kaume naye aliiomba
jamii kudumisha amani haswa katika
mda huu ambao nchi ya Kenya ipo
katika kipindi cha mpito.
Kaume alisema kuwa sababu kubwa
inayochangia katika kuvuruga amani
katika maeneo ya Shimba Hills ni
mzozo uliopo baina ya binadamu na
wanyama pori jambo ambalo
limekuwa mazoea kwa muda.
Kaume alisema kuwa ndovu
wamesababisha watu kuhama
makaazi yao wakihofia kushambuliwa
na wanyama hao. Vile vile, Kaume
alizidi kuwaomba wanaohusika na
kulinda wanyama pori kuwajibika
katika kuona kuwa kuna maisha ya
amani kati ya binadamu na wanyama
pori wanaoishia katika mbuga ya
wanyama ya kitaifa ya Shimba Hills.
W
ambalo lilijengwa na baraza la kaunti ya Kwale ili wakulima
wapate kufaidika zaidi.
Katika baraza yiyo hiyo, kamishna Achoki aliyasifu
mazingira ya Shimba Hills akisema kuwa sehemu hii ina
uwezo wa kupata mavuno ambayo yanaweza kuipiga
marufuku njaa katika maeneo hayo.
Pia, alitambua kuwa mbinu bora za kilimo ndizo
zitakazowafanya wakulima kupata mavuno mengi na
kujikomboa kutokana na hatari ya kukumbwa na baa la
njaa.
Kamishna Achoki pia alitambua hima ya wakulima katika
kutaka kuimarisha kilimo chao kwa kutumia mbolea.
Hata hivyo, alisema kuwa hata yeye anaunga mkono
mapendekezo ya wakulima kuhusu kutaka kuondolewa
mzigo wa kusafirisha mbolea toka Kwale hadi Shimba Hills.
“Niko tayari kutilia pondo juhudi za kuimarisha kilimo katika
maeneo haya kwani natambua juhudi zenu mnazozitia
katika kilimo ili kuzalisha chakula Shimba Hills” alisema.
Fauka ya hayo, kamishna huyo aliwatambua ndovu na
wanyama pori wengine kuwa ndio wanaokwaza juhudi za
wakulima katika kupata mavuno ya kutosha katika sehemu
hiyo. Kila mwaka, wakulima hupoteza mimea na mazao yao
kutokana na uharibifu wa wanyama pori.
Stage View Café
At Kinango Petrol Station—Kinango town
Serves all types of:
Cuisine, Nyama choma, Kuku choma
and
Fresh juice is also available
Eat in comfort at our cool open air premises
We offer outside catering services
Kiegezo cha kisasa cha kusimamia meli. Kitapanua biashara ya uvuvi wa samaki Katika kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla
8
Sauti Ya Pwani
Ahitaji msaada kugharamia uuguzi
Kutoka uk. Wa 1
Abdalla, ambaye ana umri wa miaka 36,
mwanzo kabisa alianzwa na ishara za
ugonjwa huu kwenye mguu wake wa
kushoto lakini ugonjwa huu ulienea kwa
haraka hadi sehemu za juu ya mguu huo.
Ishara zinazidi kuonyesha kuwa huenda
ugonjwa huu ukasambaa hadi kwenye
mguu wake wa kulia ambao tayari
umeanza kufura pia.
Abdalla ambaye alikuwa mwelekezaji
watalii, alilazimika kuwacha kazi hiyo
kutokana na jinamizi la ugonjwa jambo
ambalo lilimzidishia matatizo ya kumudu
gharama za matibabu na zile za kulisha
jamii yake.
Akizungumza na waandishi wetu, Abdalla
alidokeza kuwa alijigundua kuwa na
matende siku moja alipokuwa akila chakula
cha mchana na rafiki zake kwenye
mkahawa. Kisha akahisi maumivu makali
na kwa ghafla kupoteza ufahamu.
Akapelekwa hospitali.
“Nililazwa katika hospitali kuu ya
Msambweni kwa siku tano. Hapo ndipo
nilipogundua kuwa na matende baada ya
kuchunguzwa na madaktari,” akawaeleza
waandishi hawa.Abdalla alipelekwa
kwenye Kituo cha uchunguzi wa matibabu
cha KEMRI huko Kwale ambako uchunguzi
zaidi wa kina ulifanywa na hata akawekwa
kwenye mradi wa kuchunguza wagonjwa
wa aina yake ambapo alikuwa akipewa
vidonge vitatu kila mwaka.
Alijitosa kwenye biashara za matatu kama
manamba lakini hali yake ya afya ilizidi
kuzorota, huku akihisi maumivu mengi kila
uchao na uvimbe nao ukiongezeka kwa
kasi zaidi.
Ilimlazimu kuwacha kazi kabisa kwa
hangeweza kusimama kwa masaa mengi
kama inavyohitajika katika kazi za
manamba, na akaanza kuwa mtu wa
kutegemea wasamaria wema, majirani,
ndugu na marafiki ili kumudu maisha.
Abdalla ana matumaini ya kuishi maisha
bora hata baada ya kuukata ule mguu
mbovu kwani atakuwa na uwezo wa
kutembea kwa urahisi akitumia mguu
mmoja badala ya mzigo na maumivu
anayoyapata kwa sasa inayosababishwa
na mguu huwo.
Hata hivyo inadaiwa kuwa madaktari
katika hospitali kuu ya Msamb-
weni wamedinda kumkata mguu ilhali
madaktari wa KEMRI nao wamemshauri
apate matibabu maalum jambo ambalo
kwake ni ndoto kwa sababu ya ukosefu wa
pesa licha ya hata zile za kujimudu yeye na
jamii yake.
Hivi majuzi tu, jamii na marafiki
walikusanya shilingi 14,000 na kuwasaidia
kwa sababu hata mkewe, Asha, pia hana
ajira ilhali anatarajiwa kuwatunza wana
wao wawili.
Kijana wao wa kwanza, Abubakar,
mwenye umri wa miaka 12 na aliye darasa
la nne, alibahatika kuwa na mwalimu
mkuu aliyemruhusu kuendelea na
masomo ingawa hakuwa na karo.
Hata hivyo kijana wake wa pili ambaye
ana umri wa miaka sita na ambaye yuko
kwenye shule ya vidumbule alifurushwa
kutokana na ukosefu wa karo.
Kwa vile yeye ni wa pili kupatwa na
ugonjwa huo katika kijiji chake, Abdalla
amekuwa akipata kero hasa akiona watu
wakimtenga kwa sababu ana matende.
Abdalla amejaribu kuficha mguu wake
ambao mara nyingi huwa umezibwa na
suruali ndefu na pana; Na ana desturi ya
kuvaa viatu, lakini hivi havikuweza
kupoteza kuchechemea kutokana na uzito
na maumivu ya mguu.
Kulingana na kumbukumbu za shirika la
afya ulimwenguni, (WHO) za Januari 2012
zaidi ya watu bilioni 1.3 katika nchi 72
wanatishika kupatwa na ugonjwa wa
matende, ugonjwa ambao inadaiwa
umepuuzwa.
Asilimia 65 ya watu walioambukizwa
wanaishi kwenye eneo lililochaguliwa na
WHO kusini mashariki mwa bara Asia,
asilimia 30 wako hapa Afrika na asilimia
zile zilizobakia ni wale walioambukizwa
katika maeneo mengine duniani.
Zaidi ya watu milioni 120 hapa Afrika na
Asia kwa sasa wanaugua matende; huku
zaidi ya watu milioni 40 wakiwa
wameharibika viungo na hawaishi
maiasha ya kawaida kutokana na athari za
matende, kumbu kumbu hizo zinafafanua.
Inasemekana kuwa matende kwa
kawaida huambukizwa wakati wa ujana
lakini dalili zake hujitokeza baadaye huku
uvimbe ukijitokeza Inaendelea uk. Wa
nyuma
9
Sauti Ya Pwani
HABARI KWA PICHA
Ukiukaji wa haki za
watoto waangaziwa
V
Tafakari
baada ya
vurumai
Tana Delta
Kina mama na watoto waliathirika zaidi wakati
wa machafuko ya Tana Delta
Wakiwa wamekusanyika, wake kwa waume wakitafakari kwa kwenda baada ya mashambulizi Tana Delta
Na Emmanuel Masha,
Kaunti ya Tana River
isa vinavyozidi kuongezeka
vya kuvunjika kwa ndoa
b a i n a ya j a m i i ny i n g i
zinazoishi katika Kaunti ya Tana
River ndivyo vinavyochangia
ongezeko la watoto wasiokuwa na
malezi bora, afisa mmoja wa watoto
amenukuliwa na vyombo vya
habari.
Bi. Maria Ngali ambaye ni mkuu wa
watoto wilayani Tana River anasema
kuwa visa vya watoto waliopuuzwa
visivyopungua sita huripotiwa kila
siku kwenye afisi yake lakini
akaongeza kuwa mtindo huo
umwetapakaa kote katika Kaunti
nzima.
Bi. Ngali anasema kuwa kati ya Julai
mwaka jana na Februari mwaka huu
afisi yake ilikuwa imepokea zaidi ya
visa 310, ikiwa visa 237 ni vile
v i l i v yo ku wa n a u h u s i a n o n a
kupuuzwa kwa watoto na akawaotea
kidole cha lawana wanaume.
“Wanaume wengi hapa wilayani
hujiepusha na majukumu ya kijamii,
hasa baada ya kuwataliki wake zao,”
akasema kwa masikitiko.
Akiongea na waandishi wa habari,
Bi. Ngali aliyeandamana na afisa
mwenzake, Bw. Daniel Wailti,
aliwahimiza viongozi katika sehemu
hizi, wazazi na maafisa wa serikali
kushirikiana na kuhakikisha tabia hizi
zinakoma.
“Watu wengi katika sehemu hii ni
wale wa dini ya Kiislamu ambayo
haikatazi talaka. Wakati wazazi
wanapotalakiana, ni bayana kuwa
watoto huwa
kwenye hatari ya kupuuzwa aitha
wawe watakaa na baba au mama,”
akasema.
Katika muda huo huo, akadokeza
afisa huyo, afisi yake ilipokea visa vya
wafungwa 27, 12 vyake vikihusiana
na utundikaji mimba ilhali visa tisa
vilikuwa vya kupuuzwa kwa
watoto.
Visa vingine vilivyoripotiwa
wakati huo ilikuwa pamoja na
visa vitano vya watoto wenye
mahitaji na wanaotaka malezi
bora, visa vine vya wazazi
waliokatazwa kuwaona watoto
wao, na visa vitatu vya watoto
walio na mahitaji ya karo, yatima
na kuwachwa.
Kwa bahati nzuri kuliripotiwa
kisa kimoja tu cha ndoa za
mapema ingawa kuna habari ya
ongezeko la watoto kulazimishwa
kuolewa hasa kwa jamii za
kuhamahama.
Afisa huyu alidokeza kuwa visa
hivi huwa haviwafikii kwa vile
vinashughulikiwa na jamii
pamoja na viongozi wa kidini
a m b a p o wato to wa h u s i ka
huozwa kisiri ili wafiche aibu
zinazoambatana na ndoa za
mapema kwa familia.
Bw. Waiti alisema kuwa kuna
haja ya kuanzisha kampeini ya
haraka kuhamasisha wazazi na
viongozi kuhusu sheria
zinazomtunza mtoto huku
akisema kuwa kutekeleza sheria
kiholela hakutaweza kuleta
mafanikio bora.
“Haki za watoto chini ya
kipengele cha sheria za watoto,
kipengele cha dhuluma za
kimapenzi na katiba ni sheria
ambazo zipo lakini zikifuatiliwa
bila kuwaelimisha wahusika
huenda zikawaathiri watoto hao
hao ambao zilitungwa
kuwalinda,” akasema.
Alitoa mfano mathlani kama
mzazi atapelekwa korokoroni,
watoto hawatakuwa na mtu wa
kuwalea na kusababisha kero.

Documentos relacionados

Brazil: Je, Milango ya Benki Hubaini vyuma au Rangi za Watu?

Brazil: Je, Milango ya Benki Hubaini vyuma au Rangi za Watu? tofauti kwa kila tawi au kila mlango unaozunguka… hatuna uwezo wa kudhibiti ‘ngazi ya ufungaji’ wa kila mlango ambayo huwa kati ya ngazi ya 4 mpaka 7 (huu ni wajibu wa meneja), na hii ndiyo sababu ...

Leia mais

1 Utangulizi Kitabu cha Ayubu kimepewa jina la aliye mhusika mkuu

1 Utangulizi Kitabu cha Ayubu kimepewa jina la aliye mhusika mkuu hatia naye alikuwa mkamilifu, alimcha Mungu na kuepuka ubaya. 2Alikuwa na wana saba na binti watatu, 3naye alikuwa na kondoo 7,000, ngamia 3,000, jozi 500 za maksai, punda 500, tena alikuwa na idad...

Leia mais

Mathayo-Na-Petrillo-Na-Mwakabanje

Mathayo-Na-Petrillo-Na-Mwakabanje Hili linaweza kufafanuliwa kwa jinsi vitenzi vya aina moja vilivyotumika katika baadhi ya misemo.

Leia mais